Total Pageviews

Blog Archive

Search This Blog

Arsip Blog

Ads Here

Ads Here

Recent Posts

LIVE CHART

Skip

Featured post

SIRI KUU 3 ZA KUPUNGUZA UNENE HARAKA.

   SIRI KUU 3 ZA          KUPUNGUA UNENE HARAKA! Produced and Distributed by Lon technology p.o.box ...

Contact Form

Name

Email *

Message *

JINSI YA KUTAMBUA KAMA UNENE WAKO UKO HATARINI!

.Jinsi ya kujua kama unene wako umepitiliza
Kuna kanuni iitwayo BODY MASS INDEX (BDM) ambayo humuwesha mtu kujua kama uzito wake umezidi na maisha yake yapo hatarini.  Kwa kawaida uzito wa mwili hutegemeana na kimo cha mtu, umri na jinsia. Kanuni hii (BMI) hutupatia uwiano wa uzito wa mwili wa mtu pamoja na urefu wake.

BMI = Uzito wa mwili katika kilogramu (Kg) / Urefu wa mwili katika mita za mraba (M^2).

Kutokana na kanuni hiyo, ukichukua uzito wa mwili wako katika vipimo vya kilogramu, ukagawanya na urefu wa mwili wako katika vipimo wa mita, utapata namba ambayo kitaalamu itakuwezesha kujua kama uzito wa mwili wako upo sawa kwa maana ya kama ni uzito mkubwa au mdogo.

Mfano; mimi nina urefu wa Mita  1.75 na nina uzito wa kilogram 70kg.
Hivyo itakuwa hivi;
BMI= uzito (Kg) ÷ Urefu² (m2)
BMI = 70Kg ÷ (1.75m×1.75m)
= 70kg÷ 3.0625m²= 22.86kg/m² (uzito unaofaa)
BMI huwa na viwango mbalimbali vilivyowekwa na shirika la Afya duniani (WHO) kutafsiri hali ya lishe ya mtu ambavyo ni;
·        BMI chini ya 18.5 = uzito pungufu.(under weight)
·        BMI kati ya 18.5- 24.9= uzito unaofaa.(Normal weight)
·        BMI kati ya 25.0- 29.9 = unene uliozidi.( over weight)
·        BMI ya 30 au zaidi = unene uliokithiri (Obesity)

KITABU CHA  3 ZA KUPUNGUA UNENE HARAKA KINAUNZWA ONLINE WASILIANA NASI KWA SIMU NAMBA 0717254447 WHATSAPP 0788709100
uzito wa mwili hutofautiana kutokana na umri na jinsia ya mtu, mfano uzito wa mwanamke na mwanaume hutofautiana, pia uzito wa kijana mwenye miaka 18 na mwanaume wa miaka 40 hutofautiana, hivyo hivyo mtu mrefu huwa na uzito mkubwa kuliko mtu mfupi. 
Zingatia:
- kanuni ya BODY MASS INDEX (BDM) haitumiki kwa watu wenye ulemavu wa viungo kama viwete, vilema na watu wasiokuwa na baadhi ya viungo vya mwili kama mikono na miguu
-watoto chini ya maika kumi na nane wana kipimo chao maalumu cha BODY MASS INDEX (BDM)
-kanuni hii ya BODY MASS INDEX (BDM) haitumiki wa wanawake waliotoka kujifungua ndabi ya miezi 6
-vilevile kanuni hii ya BODY MASS INDEX (BDM), haitumiki kwa wanawake wajawazito, wanawake wajawazito wana viwango vyao maalumu vya kujua ujito wao kama uko sawa umezidi.
Watu wengi huwa hawazingatii kanuni hii, na wengine hata hawaijui, hivyo basi ni muhimu kuijua kanuni hii na kuitumia mara kwa mara ili kuweza kujua kama uzito wa mwii wako uko sahihi. Anza leo na utapata matokeo mazuri hapo baadae.

KITABU CHA  3 ZA KUPUNGUA UNENE HARAKA KINAUNZWA ONLINE WASILIANA NASI KWA SIMU NAMBA 0717254447 WHATSAPP 0788709100

Post a Comment

Copyright © LON FFB. Designed by OddThemes