Total Pageviews

Blog Archive

Search This Blog

Arsip Blog

Ads Here

Ads Here

Recent Posts

LIVE CHART

Skip

Featured post

SIRI KUU 3 ZA KUPUNGUZA UNENE HARAKA.

   SIRI KUU 3 ZA          KUPUNGUA UNENE HARAKA! Produced and Distributed by Lon technology p.o.box ...

Contact Form

Name

Email *

Message *

SIRI KUU 3 ZA KUPUNGUZA UNENE HARAKA.







   SIRI KUU 3 ZA          KUPUNGUA

UNENE HARAKA!






Produced and Distributed by
Lon technology
p.o.box 3114
Dar es salaam
Tel- 0717254447
Email-loncompany@yahoo.com














ALL RIGHTS RESERVED. Any unauthorized reprint or use of this material is prohibited. No part of this article may be reproduced or transmitted in any form or by any means, electronic or mechanical, including photocopying, recording, or by any information storage and retrieval system without express written permission from the author 

            YALIYOMO            
                                         kurasa  
1.  unene ni nini?...................1
2.jinsi ya kupima unene...........3
3. chanzo cha unene.................9
4.matatizo ya unene................16
5.makosa 6 ambayo watu hufanya katika kupunguza unene..........21
6.Siri kuu 3 za kupungua unene haraka.......................................28
6.1 chakula................................29     
i.jinsi ya kupangilia mlo wako....31
ii.mambo ya kuzingatia.............35
6.2 mazoezi...............................38
i.faida za mozoezi.....................39
ii) aina za mazoezi utakayoweza kufanya mwenyewe.............................................40
ii)mazoezi ya kufundishwa  (gym)...............46
iii)mazoezi maalumu kwa ajili ya kupunguza tumbo (kitambi)...........................................47
iv) mambo ya kuzingatia...........................54
6.3 Mtindo wa maisha (life style).............56

67. hitimisho


 1.
UNENE NI NINI?








1.Unene ni nini?

Unene ni tatizo la kiafya linalotokana na mafuta kuongezeka mwilini katika kiwango kisicho cha kawaida, hali ambayo inahatarisha afya ya muhusika na inaweza kumsababishia kifo. Tatizo hili hotekea wakati ambapo nishati (chakula) Kinachoingia mwilini ni kubwa kuliko nishati inayotoka, hii inamaanisha mtu anakula chakula kingi kuliko kazi anazozifanya.  Hali hii ya kukosekana kwa usawa wa nishati husababisha nishati iliyozidi mwilini kurundikana na kuzalisha mafuta ambayo husababisha unene. Mfano mtu anayefanya kazi  ngumu au kazi za kutumia akili nyingi anatakiwa ale zaidi kuliko mtu ambaye anashinda nyumbani akiangalia Luninga, kwa Sababu Yule anayefanya kazi nyingi mwili wake unatumia nishati nyingi hivyo kuzuia mlindukanao wa chakula kisichohitajika mwilini





      2.
JINSI YA KUPIMA KIWANGO CHA UNENE WAKO




2.Jinsi ya kujua kama unene wako umepitiliza
Kuna kanuni iitwayo BODY MASS INDEX (BDM) ambayo humuwesha mtu kujua kama uzito wake umezidi na maisha yake yapo hatarini.  Kwa kawaida uzito wa mwili hutegemeana na kimo cha mtu, umri na jinsia. Kanuni hii (BMI) hutupatia uwiano wa uzito wa mwili wa mtu pamoja na urefu wake.
BMI = Uzito wa mwili katika kilogramu (Kg) / Urefu wa mwili katika mita za mraba (M^2).


Kutokana na kanuni hiyo, ukichukua uzito wa mwili wako katika vipimo vya kilogramu, ukagawanya na urefu wa mwili wako katika vipimo wa mita, utapata namba ambayo kitaalamu itakuwezesha kujua kama uzito wa mwili wako upo sawa kwa maana ya kama ni uzito mkubwa au mdogo.
Mfano; mimi nina urefu wa Mita  1.75 na nina uzito wa kilogram 70kg.
Hivyo itakuwa hivi;
BMI= uzito (Kg) ÷ Urefu² (m2)
BMI = 70Kg ÷ (1.75m×1.75m)
= 70kg÷ 3.0625m²= 22.86kg/m² (uzito unaofaa)
BMI huwa na viwango mbalimbali vilivyowekwa na shirika la Afya duniani (WHO) kutafsiri hali ya lishe ya mtu ambavyo ni;
·        BMI chini ya 18.5 = uzito pungufu.(under weight)
·        BMI kati ya 18.5- 24.9= uzito unaofaa.(Normal weight)
·        BMI kati ya 25.0- 29.9 = unene uliozidi.( over weight)
·        BMI ya 30 au zaidi = unene uliokithiri (Obesity)


uzito wa mwili hutofautiana kutokana na umri na jinsia ya mtu, mfano uzito wa mwanamke na mwanaume hutofautiana, pia uzito wa kijana mwenye miaka 18 na mwanaume wa miaka 40 hutofautiana, hivyo hivyo mtu mrefu huwa na uzito mkubwa kuliko mtu mfupi.
Zingatia:
- kanuni ya BODY MASS INDEX (BDM) haitumiki kwa watu wenye ulemavu wa viungo kama viwete, vilema na watu wasiokuwa na baadhi ya viungo vya mwili kama mikono na miguu
-watoto chini ya maika kumi na nane wana kipimo chao maalumu cha BODY MASS INDEX (BDM)
-kanuni hii ya BODY MASS INDEX (BDM) haitumiki wa wanawake waliotoka kujifungua ndabi ya miezi 6
-vilevile kanuni hii ya BODY MASS INDEX (BDM), haitumiki kwa wanawake wajawazito, wanawake wajawazito wana viwango vyao maalumu vya kujua ujito wao kama uko sawa umezidi.
Watu wengi huwa hawazingatii kanuni hii, na wengine hata hawaijui, hivyo basi ni muhimu kuijua kanuni hii na kuitumia mara kwa mara ili kuweza kujua kama uzito wa mwii wako uko sahihi. Anza leo na utapata matokeo mazuri hapo baadae.


   3.
 CHANZO CHA     UNENE



3.Chanzo cha unene
Siku zote ukitaka kutatua tatizo lazima ujue chanzo cha tatizo hilo, kutokujua chanzo kutakufanya upoteze mda mwingi na kushindwa kutatua hilo tatizo. Hivyo basi unapoamua kutatua tatizo lako la unene ni vyema ukafahamu chanzo cha  tatizo. Vyanzo  vya tatizo la unene ni kama vifuatavyo:

i). Ulaji wa vyakula venye calories nyingi,
 ulaji wa nyakula venye karolies nyingi na venye sukari nyingi na mafuta yanayoganda husababisha mlundikano wa mafuta na kuongezeka kwa kwa unene, vyakula vilivyopikwa kwa viungo vingi kukaangwa sana huwa na kiwango kidogo cha virutibisho na kiwango kikubwa cha mafuta na sukari.
Mfano wa vyakula hivyo ni nyama nyekundu, chips, nyama choma, vyakula vyenywe sukari nyingi kama keki, bagger, pizza.

ii) Ulaji wa vyakula vya viwandani
ulaji wa vyakula vilivyosindikwa husababisha kurundikana kwa mafuta na sukari mwilini hivyo kusababisha unene, mara nyingi vyakula vilivyosindikwa huwa na mafuta mengi na sukari na hujanzwa landa nyingi ili kumvutia mlaji, mfano wa vyakula hivyo ni kama soda, biskuti, pipi, Big G, juisi, ice cream, keki na vyakula vyote vya makopo

iii) matumizi ya madawa
matumizi mabaya ya madawa kama vile madawa ya kuongeza hips, makalio, kifua na matiti huweza kusababisha kuongezeka kwa uzito na unene wa kupindukia, pia madawa kutibu magonjwa mbalimbali kama pressure , madawa ya kuzui mimba, madawa ya kuongeza kinga ya mwili nayo pia yanaweza kusababisha kuongezeka kwa mafuta na uzito. Baadhi ya dawa zenye madhara ya kuongeza unene ni kama corticosteroids, blood pressure medications, tricyclic medications na kadhalika


  iv) Umri 
 Watu wengi huongezeka uzito au hunenepa kadri umri unavyoongezeka kwa sababu wanakuwa hawajishughulishi sana (less active) na huwa wanapungua maumbile ya miili yao (muscles mass)

iv) unywaji pombe na uvutaji sigara
unywaji mwingi wa pombe huvuruga kiwango cha insulin mwilini hivyo kusababisha kuongezeka kwa sukari na uzito mwilini, pia pombe ina calories nyingi ambazo huchangia kuongezeka kwa uzito. uvutaji wa sigara husababisha mwili kushindwa kuweka uwiano sawa wa sukari mwilini hivyo kusabisha kuongezeka kwa uzito mwilini

v) msongo wa mawazo
Msongo wa mawazo na majukumu mengi husabibsha mwili kuzalisha homoni iitwayo cortisol , homoni hii huongeza kiwango cha mafuta kinachochukuliwa mwilini na pia hutanua seli za mafuta na hivyo kusabisha kuongezeka kwa mafuta mwilini na uzito, pia msongo wa mawazo husabisha watu wengine kula sana ili kujiliwaza hali inayosabisha kunenepa



vi).mtindo wa maisha.
 mtindo wa maisha kama kulala sana, kutokufanya mazoezi, kula kwa mda usiotakiwa, uvivu, kukaa sehemu moja mda mrefu, kupenda kula sana, kulala mda mfupi, kauangalia luninga mda mrefu, kutokujishughulisha vinasabisha nishati kuziti mwilini na hivyo kusababisha mwili kuongezeka uzito na kunenepa.


vi) magonjwa na matatizo ya kurithi
 Baadhi ya magonjwa yanachangia kuongezeka kwa uzito au kenenepa kama cushings syndrome, hypothyroidism, osteoarthritis na kadhalika, pia ukiwa na kiwango kikubwa cha homeni ya testosterone na ukiwa na asili ya umbo la tufaa(apple) basi unauwezekano mkubwa na kupatwa na uzito mkubwa, pia magonjwa kama ya kisukari ambayo husabisha kiwango cha sukari kuzidi mwilini husabisha kuongezejka kwa uzito, pia mmeng,enyo mbaya wa chakula tumboni husabisha kuongezeka kwa uzito









5.
MATATIZO YA UNENE

ILI KUWEZA KUSOMA KITABU CHOTE TAFADHALI NUNUA KWA TSH 5000 TU. WASILIANA NASI KWA SIMU NAMBA 0717254447, 0788709100 AU 0768359750

Post a Comment

Copyright © LON FFB. Designed by OddThemes